MWANASAIKOLOJIA CHRIS MAUKI ANENA
Mtaalamu wa Saikolojia na Uhusiano ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam, Dk. Chris Mauki, alisema kuwa picha za Mbowe akimbusu
mkewe hadharani zimemuongezea thamani kijamii kwa sababu watu
wanawapenda wanaume wanaobeba majukumu ya kifamilia.
“Unadhani kwa nini Obama ni kiongozi mashuhuri sana duniani na
anapendwa sana na watu, ni kwa sababu ya ile tabia yake ya kuwa karibu
na familia yake. Kuna watu wanampenda Obama si kwa sababu ya nguvu kubwa
aliyonayo kisiasa, ni kwa sababu anajipambanua kuwa baba bora wa
familia.
“Jamii kubwa sasa inakosa upendo wa wazi kutoka kwa akina baba. Akina
baba wengi wanaona kumbusu mkewe hadharani na kuwa karibu na familia
siyo suala lenye maana kubwa, kwa hiyo wale ambao wanayafanya hayo
waziwazi huonekana mashujaa.
“Mbowe anapongezwa kwa sababu ni shujaa kwenye jamii kwa sababu
alichokifanya wengi hawakifanyi. Familia nyingi zinakosa upendo na
kufanya mpaka watoto kuathirika kisaokolojia, watoto wanaharibika,”
alisema Dk. Mauki na kuendelea:
“Viongozi wa kisiasa wanapokuwa wanajali familia zao, inatia hamasa
kubwa. Hata kama nyumbani hawajibiki vizuri kifamilia lakini kwenye
jamii anapokuwa muwajibikaji na watu wanamuona, huvutia wengi na
kupendwa sana.”
No comments:
Post a Comment